.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 4 Desemba 2014

KAMANDI YA JESHI LA MAREKANI YABAINI IS KUPEWA MAFUNZO LIBYA

Kamandi ya Jeshi la Marekani katika bara la Afrika imesema wapiganaji wa kundi la Dola ya Kiislam (IS) wameanzisha kambi za mafunzo mashariki mwa Libya.

Jenerali David Rodriguez amesema kuna mamia ya wapiganaji wa IS ambao wanapatiwa mafunzo kwenye kambi hizo.

Amesema kuwa kambi hizo ndio kwanza zimeanza kutoa mafunzo, na Marekani inazifuatilia kuona namna zitakavyoendelea.

Nchi ya Libya imetumbukia katika machafuko tangu kiongozi wa taifa hilo Muammar Gaddafi ang'olewe madarakani na kuuwawa mwaka 2011, huku makabila kadhaa, wapiganaji na wanasiasa wakigombea madaraka.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni