.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 5 Desemba 2014

MAANDAMANO YAZIDI KUSAMBAA KATIKA MIJI KADHAA NCHINI MAREKANI

Maandamano yameendelea kufanyika kwa siku ya pili kufuatia kifo cha mwanaume mweusi kilichotokana na kukabwa kooni na polisi mweupe Jijini New York.

Maelfu ya watu wameingia barabarani Jijini New York, pamoja na katika miji mingine ya Marekani na kusababisha foleni na watu kukaa barabarani.

Maandamano hayo yaliyoanza Jumatano, baada ya mahakama kuamua kutomfungulia mashtaka askari aliyemuua Eric Garner, kwa kumkaba koo.

Wanaharakati wamewekeza matumaini yao katika uamuzi wa serikali ya jimbo kutaka kufanyika uchunguzi wa tukio hilo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni