Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya
Hifadhi ya Mji Mkongwe Zanzibar Nd. Said Sarboko Makarani
akimfahamisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif hatua
zilizochukuliwa za kuheshimu hifadhi ya urithi wa Kimataifa wakati wa
ujenzi wa Hoteli ya Park Hyatt iliyopo Forodhani Mjini Zanzibar.
Nyuma ya Nd. Sarboko ni Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mh. Abdulla
Mwinyi, Kulia ya Balozi ni Naibu Waziri wa Ardhi, Maji Nishati na
Madini Mh. Haji Mwadini pamoja na Mratibu wa Mradi wa Hoteli ya Park
Hyatt Bwana Yaqoub Osman.
Balozi Seif akikagua moja ya vyumba
vya watu Mashuhuri { VIP } kwenye Hoteli ya Park Hyatt na kuridhika
na kiwango kilichofikiwa. Hoteli hiyo inatarajiwa kufunguli wa rasmi
kwenye shamra shamra za maadhimisho ya sherehe za kutimia miaka 51
ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar zinazotarajiwa kuanza rasmi mapema
mwezi ujao wa Januari 2015.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi
ya Mji Mkonhwe Zanzibar Nd. Said Sarboko Makarani akikagua hitimisho
la ujenzi wa Hoteli ya Kimataifa ya Park Hyatt hapo Forodhani Mjini
Zanzibar.



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni