.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 5 Desemba 2014

VIONGOZI WA AFRIKA KUSINI WATAKIWA KUFUATA MISINGI YA MZEE MANDELA YA KUWAUNGANISHA WANANCHI

Aliyekuwa Naibu Rais wa Afrika Kusini, Phumzile Mlambo-Ngcuka anaamini kuwa uongozi wa Nelson Mandela kama kiunganisha wa kisiasa unahitajika hivi sasa Afrika Kusini kuliko wakati wowote ule.

Mlambo-Ngcuka ambaye hivi sasa ni Mkurugenzi wa Wanawake katika Umoja wa Mataifa amewataka wanasiasa kufuata misingi ya Madiba katika kushughulikia mambo yanayowagawa wananchi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea uhusiano wa umoja huyo na Mandela na kumbukumbu alizoacha wakati dunia ikiadhimisha mwaka mmoja tangu kiongozi huyo afariki dunia.

Uhusiano na Mandela uliimarishwa zaidi na Umoja wa Mataifa, pale wakati Baraza Kuu la umoja huo lilipotangaza Julai 18, kuwa siku ya Kimataifa ya kumuenzi Mzee Nelson Mandela.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni