Watu watano wamefariki dunia katika
tukio la moto lililotokea jana usiku katika makazi duni ya Kibera,
Jijini Nairobi.
Watu wengine watatu wapo mahututi
katika hospitali ya taifa ya Kenyatta, kufuatia janga hilo la moto
lililoanza katika moja ya nyumba.
Polisi wamesema moto huo ulianza saa
majira ya saa nne usiku na kuunguza zaidi ya nyumba 100, huku mamia
ya watu wakiachwa bila makazi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni