Miili miwili ya kwanza kutoka ndege
ya AirAsia namba QZ8501 iliyoanguka imewasili katika mji wa Surabaya
nchini Indonesia ambako ndugu wanangojea.
Ndugu wa karibu wameomba kufanyiwa
vipimo vya DNA, ili kusaidia kubaini miili ya ndugu zao waliokufa.
Ndege hiyo aina ya A320-200, ikiwa
na abiria 162 wakitokea Surabaya kwenda Singapore, ilitoweka siku ya
jumapili, na mabaki yake kuonekana baharini siku ya jumanne.
Mamlaka ya Indonesia imesema miili
saba zaidi imeopolewa, lakini zoezi hilo limeathiriwa mno na hali
mbaya ya hewa.
Miili hiyo ikiwa imebebwa kwenye majeneza yaliyopewa namba 001 na 002
Awali miili hiyo ilisafirishwa kwenye mifuko ya plastiki kutoka baharini hadi katika uwanja wa ndege wa karibu wa jeshi, na kisha kuwekwa kwenye majeneza ya mbao.



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni