Rais wa Gambia amesema bado
anashikilia mamlaka na taifa hilo la Afrika Magharibi, baada maafisa
usalama wake kuzima jaribio la kumpindua.
Rais Yahya Jammeh amesema kamanda wa
zamani wa jeshi alitaka kutwaa madaraka ya nchi hiyo kwa nguvu wakati
akiwa ziarani nchini Ufaransa, hata hivyo hatma ya kamanda huyo
haijulikani.
Awali kulikuwapo na milio mizito ya
risasa karibu na Ikulu ya rais huyo katika mji mkuu.
Rais Jammeh alitwaa madaraka ya
Gambia kwa mapinduzi mwaka 1994, na wakosoaji wake wanamlaumu kwa
kuiongoza nchi hiyo kwa utawala wa mkono wa chuma.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni