Mjadala unaokuwa kwa kasi iwapo
Idris Elba awe muigizaji wa kwanza mweusi kuigiza nafasi ya James
Bond, umeonekana kuungwa mkono na mmoja wa rapa maarufu wa Marekani
Kanye West.
Rapa huyo muongeaji mno, amesisitiza
kuwa Idris ni chagua sahihi kuchukua jukumu la kumbadili Daniel
Craig, na kazi hiyo itakuwa ni ya maono makubwa.
Kanye ameliambia gazeti la The Sun,
kuwa anamjua Idris kiasi na ni mtu mwenye kipaji kikubwa cha
uigizaji, na filamu alizoigiza ni kali na jukumu la James Bond likija
yeye anafaa.
James Bond wa sasa Daniel Craig


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni