Watu wapatao wawili jana jioni
wamejeruhiwa nchini Kenya, baada watu wasiofahamika kuwarushia bomu
la mkono katika mgahawa wa chakula katika mji wa Garissa.
Akithibitisha tukio hilo Kamishna wa
Kaunti ya Garissa Rashid Khator amesema watu hao wamepata majeraha
madogo, ambapo kundi la al-Shabaab linahisiwa kuhusika na tukio hilo.
Mashuhuda wa Tukio hilo lililotokea
eneo la Bula Adaan, wamesema watu waliojeruhiwa walikuwa nje ya
mgahawa huo, wakati watu wasiojulikana walipowarushia mlipuko huo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni