Nchi za Zambia na visiwa vya Cape Verde zimejikuta zikiondoka katika michuano ya kuwania kombe la Mataifa Afrika, baada timu hizo kutoka uwanjani zikiwa hazijafungana katika mchezo uliochezwa jana.
Mchezo huo wa kukamilisha ratiba ya kundi B ulichezwa huku mvua kubwa ikiwa inanyesha uwanjani.
Timu hizo zimejikuta zinaondoka baada ya kumaliza hatua ya makundi zikiwa za mwisho, Zambia ikiwa mkiani na pointi 2 nao Cape Verde wakiwa nafasi ya tatu na pointi 3.
Mshambuliaji wa Cape Verde Ryan Mendes ( kushoto ) akichuana na Stopilla Sunzu wa Zambia katika mchezo huo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni