.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 6 Januari 2015

CHAMA CHA WAZAZI KENYA CHATAKA SERIKALI KUWAADHIBU WALIMU WALIOGOMA

Chama cha Taifa cha Wazazi nchini Kenya kimeitaka serikali kuchukua hatua kali dhidi ya walimu waliogoma, na kusema wanakaidi amri ya mahakama inayowataka kusitisha mgomo wao huo.

Mwenyekiti wa chama hicho, Bw. Nathan Barasa, ametahadharisha kuwa uwezo wa mahakama utadharauliwa iwapo walimu wanaoendelea kukaidi amri ya mahakama hawatoadhibiwa, kwa ukaidi.

Aidha, Bw. Barasa amesema vyama vya walimu nchini Kenya ni kama vimewafanya mateka wazazi na wanafunzi, kutokana na kutumia visivyo mamlaka waliyonayo kwa walimu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni