.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 2 Januari 2015

IDADI YA MAGARI YANAYOCHOMWA MOTO USIKU WA MWAKA MPYA YAPUNGUA NCHINI UFARANSA

Serikali ya Ufaransa imesema idadi ya magari yanayochomwa moto nchini humo katika usiku wa mwaka mpya imepungua mno.

Uchomaji moto magari umepungua kwa asilimia 12, ikilinganishwa na mwaka 2013, matukio ambayo yamekuwa ni desturi kufanyika kila mwaka usiku wa mwaka mpya tangu, kutokea kwa ghasia za mwaka 2005 katika kitongoji kimoja Jijini Paris.

Idadi ya magari yaliyochomwa moto usiku wa mwaka mpya imeshuka kutoka magari 1,067 mwaka uliopita hadi kufikia magari 940 usiku wa kuukaribisha mwaka mpya wa 2015, hali iliyochangiwa na ulinzi mkali uliokuwepo kudhibiti uchomaji moto magari.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni