.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 2 Januari 2015

WANAHARAKATI WASEMA WATU WENGI WAMEUAWAWA SYRIA MWAKA 2014

Wanaharakati wamesema kuwa mwaka 2014 ulikuwa ni mwaka mbaya kwa nchi ya Syria katika miaka minne ya machafuko nchini humo ambayo yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 76,000.

Shirika la Uangalizi wa Haki za Binadamu lenye Makao yake Uingereza, limesema raia 17,790 wameuwawa nchini Syria wakiwemo watoto 3,501.

Wakati huo huo zaidi ya watu 15,000 wamekufa katika mapigano nchini Irak mwaka 2014 na kufanya mwaka jana kuwa mwaka mbaya kuwahi kutokea tangu mwaka 2007.

Vingi vya vifo na machafuko hayo vimechangiwa na wapiganaji wa kundi la Dola ya Kiislam pamoja na vikundi vingine vya wanamgambo katika nchi za Syria na Irak.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni