.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 11 Januari 2015

KIJANA MWENYE ASILI YA MALI AGEUKA SHUJAA UFARANSA BAADA YA KUNUSURU MAISHA YA WATU 15

Kijana mmoja mwenye asili ya Mali ambaye ni Muislam amepongezwa kuwa ni shujaa, baada ya kuwaficha wateja kwenye jokofu katika duka la Wayahudi, Jijini Paris ambalo lilivamiwa na mtu mwenye silaha katika moja ya matukio ya ugaidi nchini Ufaransa.

Raia huyo Lassana Bathily, 24, ambaye mfanyakazi katika duka hilo, aliwaongoza wateja waliojawa na hofu katika majokofu makubwa ya duka hilo la Hyper Cacher lililopo Porte de Vincennes, Jijini Paris.

Tangu kufanya tukio hilo la kufikiri haraka kuzima majokofu hayo na kuwaingiza wateja 15 na kuwanusuru na kifo kutoka kwa mtu mwenye silaha Amedy Coulibaly ambaye aliuwawa baadae, Bathily amekuwa akipokea pongezi nyingi.
                                  Polisi wakivamia duka Hyper Cacher kuwaokoa mateka
                           Watu waliookolewa wakitoa huku wakiangua vilio kwa hofu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni