Meya wa Jiji la New York amewakosoa
vikali mamia ya polisi wa jiji hilo ambao waligeuka na kumpa mgongo
wakati akiongea katika maziko ya maafisa polisi wawili.
Meya Bill de Blasio amesema kitendo
cha kumsusia kiongozi mbele ya umma ni sawa na kutoonyesha heshima
kwa familia za askari hao waliokufa na kwa jiji hilo.
Maafisa polisi Wenjian Liu na Rafael
Ramos walipigwa risasi na kufa mwezi uliopita na mtu mwenye silaha
aliyekuwa akilipa kisasi kwa polisi.
Maafisa wengi wa polisi wamekuwa
wakipinga kitendo cha meya huyo, kuonyesha huruma kwa waandamanaji
wanaopinga vitendo vya polisi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni