.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 6 Januari 2015

WANAUME WAWILI WAFUNGULIWA MASHTAKA MAREKANI KWA KUTAKA KUIPINDUA GAMBIA

                                                                   Rais Yahya Jammeh wa Gambia 
 
Wanaume wawili wamefunguliwa mashtaka nchini Marekani kwa kujaribu kumg'oa madarakani rais wa Gambia, Yahya Jammeh, idara ya sheria ya nchi hiyo imesema.

Washtakiwa hao ambao wanaasili ya Gambia, wanatuhumiwa kwa kula njama za kuleta madhara kwa taifa rafiki, pamoja na njama za kumiliki silaha.

Mamlaka za Gambia zimesema zimefanikiwa kuzima jaribio la kuipindua serikali lililofanywa Desemba 30, mwaka jana.

Rais Jammeh alichukua madaraka katika taifa hilo dogo la Afrika Magharibi, mwaka 1994, na amekuwa akilalamikiwa kwa kujipatia mamlaka makubwa mno.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni