.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 9 Januari 2015

POLISI PARIS WAFANYA MSAKO MKUBWA KUWASAKA WAUAJI WAWILI NDUGU

Operesheni kubwa ya polisi inafanyika kaskazini mashariki mwa Paris katika kuwatafuta watuhumiwa wakuu wa mauaji yaliyotokea jumatano, katika ofisi za jarida la vibonzo la Charlie Hebdo.

Maafisa polisi wanafanya msako katika maeneo karibu na mji wa Villers-Cotterets ambao watuhumiwa hao wawili ndugu waliouwa watu 12, waliripotiwa kuiba katika kituo cha mafuta.

Wanakijiji wa kijiji cha Longpont walizuiliwa kutoka wakati wa msako wa nyumba kwa nyumba unaowatafuta wauaji hao ndugu Cherif na Said Kouachi.
                      Wanaume wakiwa kazini kuwasaka wahalifu Cherif na Said Kouachi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni