Watu wapatao wawili wamekufa na
wengine kadhaa wakijeruhiwa jana usiku baada ya jengo la ghorofa sita
la makazi kuanguka katika makazi ya Huruma Jijini Nairobi.
Mtu mmoja alikufa wakati akiwasili
hospitali ya Kenyatta, wakati huo huo mwili wa mtoto ukitolewa kwenye
kifusi, kwa mujibu wa maafisa wa kitendo cha taifa cha kukabiliana na
majanga Kenya.
Maafisa wa Jiji la Nairobi wamesema
watu 22 wamenusurika baada ya kutolewa kwenye vifusi vya jengo hilo,
hata hivyo haijulikani ni watu wangapi bado wapo kwenye jengo hilo
lililoanguka.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni