.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 19 Februari 2015

MASHAMBULIZI YA ANGA YAUWA WAOMBELEZAJI KUSINI MWA NIGER

Watu 37 wamekufa katika mashambulizi ya anga yaliyofanywa kusini mwa Niger kwa kundi la watu waliokuwa mazishi.

Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Abadam kinachopakana na Nigeria, ambapo ndege ambayo haijafahamika ni ya nchi gani ilipowadondoshea mabomu.

Hali hiyo imetokea wakati Nigeria ikisema zaidi ya wapiganaji 300 wameuwawa karibu na kusini-mashariki mwa Nigeria katika operesheni ya kutokomeza kundi la Boko Haram.

Wakati huo huo wanajeshi wawili wamepoteza maisha yao na wengine 10 wamejeruhiwa katika jimbo la Borno.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni