.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 19 Februari 2015

RAIS BARACK OBAMA ASEMA MAREKANI HAIPIGANI NA UISLAM

Rais Barack Obama amesema Marekani haipigani vita na Uislam, ila ipo katika vita dhidi na watu wanaofanya vitendo visivyokubalika na Uislam.

Obama ametoa kauli hiyo mbele ya wawakilishi 60 wa mataifa mbalimbali wanaohudhuria mkutano wa siku tatu wa kukabiliana na makundi yenye kufuata itikadi kali, kufuatia mashambulio ya nchini Denmark na Ufaransa.

Amesema kuwa dunia inapaswa kupambana na itikadi zinazowafanya watu kuwa na misimamo mikali yenye kuleta madhara.

Rais Obama amesema vikundi kama Dola ya Kiislam na kundi la al-Qaeda si vya kidini bali ni vya kigaidi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni