Nchi ya Liberia imemruhusu kutoka
hospitali mgonjwa wake wa mwisho aliyepona Ebola, baada ya kukaa wiki
nzima bila kupata maambukizi mapya ya Ebola.
Shirika la Afya Duniani (WHO)
limesema mgonjwa huyo Beatrice Yardolo, aliruhusiwa kutoka katika
kituo cha Ebola kinachosimamiwa na China katika Jiji la Monrovia
baada ya kutibiwa kwa wiki mbili.
Karibu watu 10,000 wamekufa kwa
ugonjwa wa Ebola wengi wakiwa ni katika nchi za Guinea, Liberia na
Sierra Leone.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni