.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 31 Machi 2015

RAIS BARACK OBAMA KUTEMBELEA KENYA MWEZI JULAI

Rais Barack Obama wa Marekani anatarajiwa kuitembelea Kenya kwa mara ya kwanza tangu awe rais katika ziara yake aliyopanga kuifanya mwezi Julai, mwaka huu na atakuwa rais wa kwanza wa taifa hilo aliyepo madarakani kutembelea Kenya.

Rais Obama mwenye asili ya Kenya, anatarajiwa kuhudhuria mkutano wa wa dunia wa Ujasiriamali wa mwaka 2015 Jijini Nairobi, ambao unaandaliwa kwa ushirikiano baina ya Kenya na Marekani.

Msemaji wa Ikulu ya Kenya Manoah Esipisu ametangaza ujio huo wa rais Obama jana mara tu baada ya Ikulu ya Marekani kuthibitisha ziara hiyo, ambayo inahusiana na tukio hilo la mkutano huo wa kila mwaka wa dunia ambao umekuwa ukifanyika tangu mwaka 2009.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni