Rais Yoweri Museveni wa Uganda
ametangaza baraza jipya la mawaziri hapo jana huku Mary
Karooro Okurut akiteuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi kuchukua nafasi ya
Muruli Mukasa.
Katika mabadiliko hayo mapya, Muruli
Mukasa sasa ni Waziri Jinsia, Ajira na Masuala ya Jamii nafasi ambayo
ilikuwa ikishikiliwa na Okurut, naye Jim Muhwezi ameteuliwa kuwa
Waziri wa Habari kuchukua nafasi ya Rose Namayanja.
Matia Kasaija amekuwa Waziri wa
Fedha na Mipango ya Uchumi na kuchukua nafasi ya Maria Kiwanuka
ambaye anakuwa ni Mshauri Mwandamizi wa rais masuala ya Fedha, pia
Peter Nyombi ameondolewa katika nafasi ya Mwanasheria Mkuu na nafasi
yake kupewa Fred Ruhindi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni