.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 5 Machi 2015

VYAMA VITANO VYA UPINZANI VYAUNDA SERIKALI YA MSETO NCHINI LESOTHO

Vyama vitano vya upinzani nchini Lesotho, vimeunda muungano mpya wa kuunda serikali baada ya uchaguzi wa dharura uliofanyika mwishoni mwa wiki kushindwa kumpata mshindi.

Uchaguzi huo uliitishwa kujaribu kuzima hali ya hofu, baada ya kuwepo jaribio la kuipindua serikali mwezi Agosti mwaka jana.

Waziri Mkuu anayeondoka madarakani wa Chama cha Basotho, Thomas Thobane amekuwa wa pili kwa kupata viti 46 katika uchaguzi huo, huku Pakalitha Mosisili wa chama cha Democratic Congress akipata viti 47 na ameungana na vyama vingine vidogo kupata viti 61.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni