.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 15 Aprili 2015

CUBA YAONDOLEWA KATIKA ORODHA YA KUFADHILI UGAIDI

Rais wa Marekani Barack Obama ( kulia ) akisalimana na Rais wa Cuba, Raul Castro. 

Ikulu ya Marekani imesema Rais Barack Obama ameiondoa nchi ya Cuba katika orodha ya mataifa ambayo yanafadhili ugaidi, ikiwa ni moja ya hatua muhimu ya kuimarisha uhusiano kati ya mataifa hayo mawili. 

Cuba iliorodheshwa kuwa moja kati ya mataifa yanayofadhili ugaidi March 01' 1982, ikiwa ni pamoja na nchi za Iran mwaka 1984, Sudan 1993 na Syria iliyowekwa katika orodha ya kufadhili ugaidi mwaka 1979. 

Serikali ya Cuba imepokea kwa mikono miwili uamuzi huo wa Rais Obama, lakini imesisitiza kuwa tangu mwanzo nchi hiyo haikustahili kuwekwa katika orodha ya mataifa yanayofadhili ugaidi kwani haikuwahi kufanya hivyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni