.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 15 Aprili 2015

WATU TISA WAKAMATWA NA SILAHA MBALIMBALI NA VIFAA VYA MILIPUKO MKOANI MOROGORO

Jeshi la polisi mkoani Morogoro linawashikilia watu tisa ( 9 ) waliokuwa wamejifungia ndani katika msikiti wa Sunni eneo la Kidatu wilayani Kilombero wakiwa na silaha za aina mbalimbali pamoja vifaa vya milipuko. 

Kamanda wa polisi mkoani Morogoro, Leonard Paul amesema katika operesheni kabambe ya kuwakamata watuhumiwa hao, askari mmoja alijeruhiwa kwa kukatwa shingo na jambia. 

Kamanda huyo amesema kukamatwa kwa watu hao kumefanikiwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema. 

Watu hao wanashikiliwa kwa mahojiano, na Kamanda Paul amesema hawezi kutaja majina yao kwa muda huu mpaka hapo upelelezi utakapokamilika.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni