.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 12 Aprili 2015

DEREVA LEWIS HAMILTON AIPATIA USHINDI TIMU YAKE YA MERCEDES HUKO CHINA

Dereva wa mbio za Langalanga Muingereza Lewis Hamilton ameipatia ushindi timu yake ya Mercedes katika mbio za Chinese Grand Prix.

Muingereza huyo bingwa wa mbio hizo wa dunia, aliongoza kwa umbali akionyesha umahiri wake na kumshinda dereva mwenzake wa timu ya Mercedes Nico Rosberg.

Madereva wa timu ya Ferrari, Sebastian Vettel pamoja na Kimi Raikkonen walionyesha ushindani lakini walizidiwa na uwezo wa timu ya Mercedes wa kumudu kubadilisha matairi.

Katika mbio hizo timu ya Williams, yenye madereva Felipe Massa pamoja na Valtteri Bottas walishika nafasi ya tano na ya sita.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni