.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 12 Aprili 2015

HOFU YA UGAIDI ZAIDI YA WANAFUNZI 100 WA CHUO KIKUU CHA NAIROBI KENYA WAJERUHIWA

Zaidi ya wanafunzi 100 wa Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya wamejeruhiwa leo alfajiri kwa kukanyagana baada ya trasfoma ya umeme kulipuka na kuibua hali ya taharuki.

Tukio hilo lililotokea majira ya saa kumi alfajiri limetokea katika kampasi ya Kikuyu, na kuibua hofu na hali ya taharuki baada ya wanafunzi wengi kudhani mlipuko huo ni tukio la kigaidi.

Hali hiyo ilipelekea wanafunzi hao kuruka kutoka juu ya ghorofa wengine hadi kutokea ghorofa ya sita ya hosteli yao katika kujaribu kujinusuru, ambapo wengi wao wamejeruhiwa vibaya.

Wanafunzi wapatao 100, wamelazwa katika hospitali ya Taifa ya Kenyatta, na wengine wamepelekwa hospitali za Mtakatifu Teresa na Karen.

Tukio hilo limetokea baada ya wiki mbili kupita tangu wanafunzi 148, kuuwawa katika Chuo Kikuu cha Garissa kwa shambulio lililofanywa na magaidi wa kundi la Somalia la al-Shabaab.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni