.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 12 Aprili 2015

PAPA FRANCIS ASEMA KILICHOFANYIKA ARMENIA NI MAUAJI YA KIMBARI

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis ametumia neno mauaji ya kimbari, wakati akielezea mauaji ya wa Armenia wengi chini ya utawala wa Ottoman wakati wa vita ya kwanza ya dunia miaka 100 iliyopita.

Matamshi hayo ya Papa ameyatoa wakati wa misa Jijini Vatican, ambapo wa Armenia pamoja wanahistoria wanasema watu milioni 1.5 waliuwawa na vikosi vya Ottoman mnamo mwaka 1915.

Hata hivyo kauli hiyo ya Papa Francis inatarajia kuibua hasira za taifa la Uturuki, ambalo limekuwa likisisitiza kuwa mauaji hayo hayakuwa ya kimbari.

Rais wa Armenia Serzh Sargsyan alihudhuria misa hiyo iliyofanyika Vatican, katika kumbukumbu ya karne ya 10 ya mauaji hayo ya wa Armenia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni