.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 10 Aprili 2015

HALI YA HOFU MIONGONI MWA WANANCHI WA MKOA WA ARUSHA IMEJITOKEZA, LEO

Hali ya hofu miongoni mwa wananchi wa Mkoa wa Arusha imejitokeza, leo asubuhi, kufuatia kusambaa kwa ujumbe mfupi kwenye mitandao ya kijamii na simu za kiganjani kuwa kuna magaidi wanne wamekamatwa na silaha aina ya SMG katika chuo cha Uhasibu Njiro (IAA).

Akizungumzia taarifa hizo,Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha, Liberatus Sabasi, amesema wananchi wanapaswa kuendelea na shughuli zao kama kawaida na kupuuza ujumbe huo.

Amesema taarifa hizo zitakuwa zimesambazwa na wahuni wachache kwa lengo wanalojuwa wenyewe, ila ulinzi wameimarisha kila mahali watu wafanye shughuli zao kama kawaida.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Daudi Ntibenda, alipopigiwa simu ya kiganjani, amesema huo ni uwongo na kila mmoja aupuuze.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni