.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 7 Aprili 2015

JAJI MAREKANI ARIDHIA KUUWAWA KWA MWANAUME ALIYEWAUWA WANAFUNZI WAISLAMU

Jaji wa North Carolina ameridhia mwanaume mmoja anayetuhumiwa kuwauwa wanafunzi watatu Waislamu nchini Marekani, apatiwe adhabu ya kifo.

Jaji Mwandamizi Orlando Hudson amesema kwamba waendesha mashtaka wanahoja kuu mbili za msingi zinazomfanya mtuhumiwa huyo Craig Stephen Hicks kustahiki kukabiliwa na adhabu ya kifo.

Craig Hicks anashtakiwa kwa mauaji ya Deah Barakat na mkewe Yusor Mohammad Abu-Salha pamoja na dada yake Razan Mohammad Abu-Salha.
                   Wanafunzi Waislamu waliouwawa wakiwa katika picha ya pamoja

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni