.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 7 Aprili 2015

WAZIRI WA ARDHI KENYA KUHOJIWA NA TUME YA KUKABILIANA NA RUSHWA

Waziri wa ardhi aliyesimamishwa kazi Charity Ngilu leo anatarajiwa kukutana na maafisa wa kukabiliana na rushwa katika jengo la Maadili Jijini Nairobi kuhojiwa kuhusiana na tuhuma za ukiukaji wa maadili.

Bi. Ngilu, ambaye amelazimishwa kuachia madaraka ili kupisha uchaguzi, alikuwa anatumia Sikukuu ya Pasaka katika kujenga utetezi wake kuhusiana na tuhuma zinazomkabili.

Msemaji wa Tume ya Maadili na Kupambana na Rushwa Kenya, Yasin Amaro, amesema kuwa pia Msajili Mkuu wa Ardhi Kenya Sarah Mwendwa naye pia ayafika mbele ya tume hiyo kujitetea hii leo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni