Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim
Jong-un ameagiza kuuwawa watu 15 katika mwaka huu wakiwemo maafisa waandamizi
kadhaa wa serikali yake.
Idara ya Upelelezi ya Korea
Kusini imekiambia kikao cha bunge hii leo kuwa watu hao wameuwawa kwa kupigwa risasi
kwa madai kuwa ni mashushushu.
Waliouwawa ni pamoja na manaibu
waziri wawili, waliopingana na Kim kuhusina na sera zake pamoja na maafisa wa
idara ya upelelezi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni