.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 29 Aprili 2015

MATAIFA YAONYESHA HASIRA BAADA YA KUUWAWA RAIA WAO NCHINI INDONESIA



Australia imemtaka balozi wake kuondoka nchini Indonesia baada ya raia wake wawili kuuwawa baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya kusafirisha dawa za kulevya.


Raia hao Andrew Chan na Myuran Sukumaran ni miongoni mwa watu wanane kutoka mataifa kadhaa waliouwawa kwa kupigwa risasi hii leo katika gereza la kisiwa cha Nusakambangan.


Serikali ya Brazil nayo imeonyesha kusikitishwa mno kutokana na kuuwawa kwa raia wake aitwae Rodrigo Gularte.


Hata hivyo mwanamke mmoja alisitishiwa adhabu ya kuuwawa baada ya kuelezwa kwamba mwanamkeambaye aliyemuwekea dawa za kulevya alikuwa anashikiliwa gerezani.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni