.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 9 Aprili 2015

MTANZANIA ANAYESHIKILIWA KENYA KWA UGAIDI KUKAA RUMANDE SIKU 30


Mtanzania anayehusishwa na tukio la shambulio la kigaidi la Chuo Kikuu cha Garissa lililouwa wanafunzi 148, ataendelea kushikiliwa kizuizini na jeshi la polisi Kenya kwa muda wa mwezi mmoja.

Mahakama moja Jijini Nairobi leo imeagiza mtanzania huyo Rashid Charles Mberesero almaarufu kama Rehani Dida, atashikiliwa pamoja na watuhumiwa wenzake watano wa shambulio hilo.

Siku ya jumanne Mberesero hakuwepo mahakamani kutokana na kusafiri kwenda Garissa akiwa na wapelelezi wanaochunguza shambulio hilo, wakati mahakama ikitoa amri kwa watuhumiwa 14 wanaodaiwa kuwa ni wa kundi la al-Shabaab wakiswekwa rumande kwa muda wa siku 30 wakisubiri uchunguzi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni