.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 5 Aprili 2015

PAPA FRANCIS ASHUTUMU MAUAJI YA WANAFUNZI WAKRISTO KENYA

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis ameshutumu mgawanyiko na kuwepo kwa ukimya dhidi ya matukio ya mashambulizi ya Jihadi dhidi ya Wakristo duniani, kauli ambayo ameitoa wakati akiongoza sherehe za Pasaka.

Kiongozi huyo wa kanisa hilo lenye waumini wapatao bilioni 1.2 amegusia suala la mauaji ya wakristo yanayofanywa na watu wenye itikadi kali za kidini, wakati kanisa likisherehekea siku kuu takatifu ya Pasaka ambayo ni ya kufufuka kwa Yesu kristo.

Katika wiki hii takatifu kwa mujibu wa kalenda ya Kanisa, wanafunzi wakristo 152 waliuwawa katika Chuo Kikuu cha Garissa nchini Kenya katika shambulio lililofanywa na kundi la kigaidi la Somalia la al-Shabaab. 
 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni