.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 6 Aprili 2015

RONALDO AFANYA KUFURU APACHIKA MABAO 5 WAKATI REAL IKIFANYA MAUAJI

Cristiano Ronaldo ameiongoza Real Madrid kufanya maangamizi baada ya kufunga hat-trick ndani ya dakika nane katika kipindi cha kwanza na kuisambaratisha Granada kwa mabao 9-1 hapo jana.

Mchezaji huyo raia wa Ureno alipachika kimiani tena mabao mawili katika kipindi cha pili na kutimiza kufunga magoli matano peke yake katika mchezo huo wa ligi kuu ya Hispania. La Liga.

Katika mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la Santiago Bernabeu, mshambuliaji wa Real, Karim Benzema alipachika wavuni mabao mawili, huku Gareth Bale akiwa wa kwanza kucheka na nyavu na kufungulia mvua hiyo ya magoli.
                                                                        Ronaldo akimtoka beki wa Granada
                                                                          Gareth Bale akipachika wavuni goli

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni