.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 6 Aprili 2015

SHIRIKA LA KIMATAIFA LA MSALABA MWEKUNDU (ICRC) KUPELEKA NDEGE YEMEN

Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (ICRC) linatarajia kupeleka ndege mbili za kutoa msaada wa dharura katika mji mkuu ya Sanaa nchini Yemen.

Shirika hilo limepewa ruhusa ya kutua ndege zake zikiwa na watumishi pamoja na dawa za matibabu nchini Yemen ambapo inaelezwa kunahitajika misaada ya dharura ya kibinadamu.

Mashambulizi ya anga yanayoonozwa na nchi ya Saudi Arabia yakiwalenga waasi wa Houth, yameendelea kufanywa kwa usiku wa 12 mfululizo.

Umoja wa Mataifa unasema kuwa zaidi ya watu 500, wameuwawa katika wiki mbili zilizopita nchini Yemen.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni