Kunataarifa zinaeeleza
kuwa baadhi ya viongozi wa jaribio la kuipindua nchi ya Burundi
lililoshindikana wamekamatwa.
Haijafahamika mara moja
iwapo Jenerali Godefroid Niyombare, aliyetangaza mapinduzi ni
miongoni mwa watu waliokamatwa.
Mmoja wa jenerali
msaliti aliyejaribu kutwaa madaraka nchini Burundi amesema anamini
jaribio lao la kutaka kumng'oa madarakani rais Pierre Nkurunziza
limeshindikana.
Jenerali Cyrille
Ndayirukiye ameliambia shirika la habari la AFP, kuwa wengi wa
wanajeshi wanataka serikali ya sasa iendelee kuwepo madarakani.
Wakati huo huo, rais wa
Nkurunziza ametwiti katika ukurasa wake wa twitta kuwa amerejea
nchini Burundi, na kunataarifa kuwa sauti yake imesikika katika redio
ya taifa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni