Jeshi la Nigeria limewauwa
wapiganaji kadhaa wa Boko Haram na kuwaokoa wanawake 20 na watoto
katika operesheni iliyofanyika kwenye msitu wa Sambisa ambao ndio
maficho pekee ya kundi hilo kaskazini-mashariki mwa nchi hiyo.
Taarifa iliyotolewa msemaji wa jeshi
Meja Jenerali Chris Olukolade, aimeeleza kuwa mwanajeshi mmoja
ameuwawa na bomu la kutega aridhini, wakati wa operesheni hiyo ambapo
wengine 10 wamejeruhiwa.
Maelfu ya watu wameuwawa na kundi la
Boko Haram katika kipindi cha miaka sita ya harakati zake za
mapambano ya kusimika utawala wenye kufuata sheria Kiislam.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni