.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 16 Mei 2015

MAHAKAMA NCHINI MAREKANI IMEMUHUKUMU ADHABU YA KIFO ALIYEHUSIKA NA MILIPUKO YA BOSTON

Mahakama nchini Marekani imemuhukumu adhabu ya kifo kwa kuchomwa sindano Dzhokhar Tsarnaev aliyehusika na tukio la milipuko ya bomu iliyotokea Boston.

Watu watatu waliuwawa katika tukio hilo na wengine 260 walijeruhiwa wakati Tsarnaev na kaka yake walipoweka milipuko ya mabomu katika eneo la kumalizia mbio za Marathoni za Boston mwaka 2013.

Inawezekana sasa Tsarnaev akapelekwa kwenye gereza la Terre Haute, Indiana, angingojea kutekelezewa adhabu hiyo, lakini kunauwezekano pia kukawa na hatua ya kukata rufaa katika mahakama za juu.

Waathirika wa tukio hilo walitokwa na machozi wakati hukumu hiyo ikisomwa lakini Tsarnaev hakuonyesha hisia zozote.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni