.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 22 Mei 2015

NCHI YA MYANMAR IMEFANIKIWA KUWAOKOA WAHAMIAJI ZAIDI YA 200 BAHARINI

Nchi ya Myanmar imefanikiwa kuwaokoa wahamiaji zaidi ya 200 kwenye boti mbili katika ukanda wake wa baharini unaopakana na Bangladesh.

Huu ni uokozi wa kwanza kufanywa na Myanmar ambayo imekabiliwa na shutuma kwa kutofanya jitihada za kutosha kusaidia wahamiaji waliokwama baharini.

Wengi wahamiaji ni kundi la waislam wa jamii ya Rohingya wanaokimbia kuuwawa Myanmar, huku wengine wahamiaji wanaoikimbia hali mbaya ya uchumi nchini Bangladesh.

Zaidi ya wahamiaji 3,000 wameingia nchi za jirani za Malaysia, Thailand pamoja na Indonesia, ambazo zimekubali kutoa msaada.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni