.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 12 Mei 2015

RAIS PIERRE NKURUZINZA WA BURUNDI AKATAA WITO WA UMOJA WA ULAYA NA MAREKANI

Rais Pierre Nkuruzinza wa Burundi amekataa wito wa Umoja wa Ulaya na Marekani wa kusitisha uchaguzi mkuu uliogubikwa na utata uliopangwa kufanyika mwezi Juni, kutokana na hali tete ya usalama.

Akiongea na vyombo vya habari vya magharibi, rais Nkuruzinza amesema iwapo uchaguzi mkuu hautofanywa kama ulivyopangwa hali itazidi kuwa mbaya zaidi kuliko ilivyo hivi sasa na kuitumbukiza nchi katika machafuko.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni