Mtaalam wa haki za binadamu wa Umoja
wa Mataifa amesema Paraguay imeshindwa kumlinda mtoto wa miaka 10
aliyebakwa, ambaye amekataliwa kutoa ujauzito.
Mtoto huyo wa kike anadaiwa kupata
ujauzito huo baada ya kubakwa na baba yake wa kambo.
Mtaalamu huyo amesema uamuzi wa
serikali ya Paraguay umevunja haki za mtoto huyo, na kutoa wito mtoto
huyo wa kike apatiwe uangalizi wa huduma za afya.
Taifa la Paraguay limepiga marufuku
utoaji wa mimba, isipokuwa pale tu ambapo maisha ya mama yapo
hatarini.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni