.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 15 Juni 2015

KAMANDA WA AL SHABAAB RAIA WA UINGEREZA AUWAWA KENYA KATIKA SHAMBULIO LA JANA

Jeshi la Kenya limesema kamanda wa kikanda wa kundi la al Shabaab la nchini Somalia ambaye pia inasadikiwa ni raia wa Uingereza aliyejiunga na wapiganaji wa kundi hilo, ameuwawa katika mapigano yaliyotokea mwishoni mwa wiki.

Wapiganaji 11 wa kundi hilo pamoja na wanajeshi wawili wa Kenya walikufa baada ya kundi hilo la al Shabaab kuvamia kambi ya jeshi la Kenya kwenye kaunti ya Lamu kaskazini mwa mkoa wa Pwani.

Msemaji wa vikosi vya Ulinzi Kenya Kanali David Obonyo amesema miongoni mwa waliouwawa ni Luqman Osman Issa ambaye pia anajulikana kama Shirwa, anayetuhumiwa kuongoza shambulio la Mpeketoni mwaka mmoja uliopita lililouwa watu 65.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni