Mawaziri wa Mambo ya Ndani wa Umoja
wa Ulaya watajadiliana jinsi ya kukabiliana na makumi ya maelfu ya
wahamiaji wanaoingia Ulaya kila mwaka kwa kukatiza bahari ya
Mediterranean.
Jambo muhimu katika mazungumzo hayo
yanayofanyika Jijini Luxembourg ni kupanga namna ya kugawana
wakimbizi hao kwa usawa katika mataifa yote 28 ya Umoja wa Ulaya.
Mzigo wa uhamiaji umeibua mgogoro
mkubwa wa rasilimali katika mataifa ya Italia, Ugiriki na Maltese.
Hata hiyo mataifa ya kaskazini na
kusini mwa Ulaya yametaka wahamiaji hao wasilazimishwe kuenda nchi
wasizotaka kwenda.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni