Viongozi wa Afrika wametoa wito wa
kuboreshwa ushirikiano wa kupambana na ongezeko la mashambulizi yenye
kufuata misimamo mikali ya kiimani katika maeneo tofauti ya bara
hili.
Kauli hiyo ya viongozi hao
wanaokutana nchini Afrika Kusini, imetolewa wakati ambapo mwana Jihad
mmoja kujilipua kwa bomu na kuuwa watu 27 katika Jiji Kuu la
N'Djamena nchini Chad siku ya jumatatu.
Tukio hilo linachukuliwa kuwa ni
kitendo cha kulipa kisasi cha wabinagaji wa kundi la Boko Haram,
kutokana na taifa la Chad kuongoza operesheni ya kijeshi ya kikanda
ya kuwasambaratisha wapiganaji wa kundi hilo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni