Mgonjwa mwingine amefariki dunia
nchini Korea Kusini kufuatia mlipuko wa ugonjwa unaoshambulia mfumo
wa hewa wa (Mers) na kufanya idadi ya waliokufa kufikia watu 16.
Maafisa pia wameripoti kuibuka kwa
maambukizi mapya matano Korea Kusini, ambayo inamlipuko mkubwa wa
ugonjwa huo katika nchi za Mashariki ya Kati.
Maafisa wa Korea Kusini wamesema
kuwa idadi ya watu 150, wameambukizwa virusi vya ugonjwa huo.
Wakati huo huo raia wa Korea Kusini
aliyepo Slovakia amebainika kuwa hana virusi, lakini ataendelea kuwa
chini ya karantini kwa ajili ya vipimo zaidi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni