.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 6 Julai 2015

MAHAKAMA YAWAHUKUMU MRAMBA NA YONA KIFUNGO CHA MIAKA MITATU JELA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo imewahukumu kifungo cha miaka mitatu jela na kulipa faini ya shilingi milioni 5 kila mmoja aliyekuwa Waziri wa Fedha Basil Mramba na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Daniel Yona baada ya kuwatia hatiani kwa makosa mawili.

Hukumu hiyo imetolewa na Jaji John Utamwa, Jaji Sam Rumwenyi pamoja na Hakimu Saul Kinemela ambapo mtuhumiwa wa tatu wa kesi hiyo, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja amekutwa hana hatia.

Washitakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na mashitaka ya matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 11.7 kutokana na kutoa msamaha wa kodi kwa kampuni ya kukagua madini ya dhahabu ya MS Alex Stewart ya Uingereza.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni