.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 6 Julai 2015

WAKAZI WA JIJI LA NAIROBI WATAKIWA KUJIANDAA KWA USUMBUFU ZIARA YA RAIS OBAMA

Wakazi wa Jiji la Nairobi na vitongoji vyake wametakiwa kutarajia usumbufu wakati wa ziara ya rais Barack Obama wa Marekani baadae mwezi huu.

Msemaji wa Ikulu Monoah Esipisu amesema baadhi ya barabara zitafungwa, hata hivyo shughuli za kawaida zitaendelea katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta.

Rais Obama anatarajiwa kutua katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta, akiwa na ndege yake ya Air Force One na baadae kuelekea Gigiri kupitia barabara ya Mombasa.

Msafara wa rai Obama utahusisha gari lake lisilopenya risasi aina ya limo lijulikanalo kama The Beast yaani Mnyama, pamoja na gari la huduma ya kwanza la kijeshi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni